* MAFURIKO MAKUBWA YATOKEA MWANZA....
Page 1 of 1
* MAFURIKO MAKUBWA YATOKEA MWANZA....
katika hali inayotafsiriwa kuwa ni ngumu kuzuia mafuriko kwa viganja vya mikono leo hii ukweli wa jambo hilo limethiirika pale Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli Ndg. Edward Lowassa alipozuru katika jiji la Mwanza kwa ajili ya kutafuta wathamini ndani ya chama chake....
Baada ya kutua msafara wa Lowassa ulipata wakati mgumu kutokana na kusimamishwa mara kwa mara na maelfu ya watu japo aweze kuwasalimu hata kwa kuwapungia mkono. Makundi hayo yalianza kukusanyika tokea asubui na mapema ya leo waliposikia waziri mkuu huyo mstaafu atapita Mwanza kwa ajili ya utafutaji wa wathamini....
"Ndugu yangu jiji limesimama kwa muda, maduka mengi yamefungwa, shughuli nyingi zimesimama, shughuli nyingi za machinga (Makoroboi) zimesimama huku wakisema wanaenda kwa rafiki yao, Bodaboda nao siku ya leo wengi wao hawajafanya kazi. Siunakumbuka hotuba ya Lowassa iliwataja haya makundi kuwa ni marafiki zake binafsi, sasa leo ndiyo kweli nimeamini hawa watu ni marafiki, kwa umoja huu walioonyesha leo ni hatari".. Mzee Masanja, amesikika akisema...
Baadhi ya wenyeji wa Mkoa huo wa Mwanza wanakiri kwamba tukio hilo na umati wa namna hiyo ni miaka kadhaa hawajawahi kushuhudia. "Ni wazi hizi nguvu sio za kawaida, wananchi wamejitokeza wengi, wengi sana. Walianza kukusanyika tokea asubui. Mimi nilikuwa sijui kuna nini ila nilipoanza kuwauliza moja moja ili nipate kujua kuna nini, wote walinijibu wamekuja katika safari ya matumaini na kweli baada ya kuona uwingi ule wa watu sina neno zaidi ya kusema HII NDIO SAFARI YA MATUMAINI"... Emmanuel..
Mafuriko haya ya watu ni kiashiria tosha ya jinsi gani wananchi wameamua kuunga mkono safari ya matumaini. Safari ambayo Nchi itapata uongozi wenye uthubutu, usioogopa kufanya maamuzi magumu, uongozi thabiti, makini na usioyumba. Uongozi wenye ubunifu na upeo mkubwa, uongozi unaoamini katika mfumo shirikishi katika ujenzi wa Taifa na uongozi unaozingatia muda katika kutekeleza majukumu yake. Ndugu yangu wakati ndio huu, njoo ujiunge na safari ya matumaini....
"HII NDIO SAFARI YA MATUMAINI, MCHAKAMCHAKA WA MAENDELEO"....
Baada ya kutua msafara wa Lowassa ulipata wakati mgumu kutokana na kusimamishwa mara kwa mara na maelfu ya watu japo aweze kuwasalimu hata kwa kuwapungia mkono. Makundi hayo yalianza kukusanyika tokea asubui na mapema ya leo waliposikia waziri mkuu huyo mstaafu atapita Mwanza kwa ajili ya utafutaji wa wathamini....
"Ndugu yangu jiji limesimama kwa muda, maduka mengi yamefungwa, shughuli nyingi zimesimama, shughuli nyingi za machinga (Makoroboi) zimesimama huku wakisema wanaenda kwa rafiki yao, Bodaboda nao siku ya leo wengi wao hawajafanya kazi. Siunakumbuka hotuba ya Lowassa iliwataja haya makundi kuwa ni marafiki zake binafsi, sasa leo ndiyo kweli nimeamini hawa watu ni marafiki, kwa umoja huu walioonyesha leo ni hatari".. Mzee Masanja, amesikika akisema...
Baadhi ya wenyeji wa Mkoa huo wa Mwanza wanakiri kwamba tukio hilo na umati wa namna hiyo ni miaka kadhaa hawajawahi kushuhudia. "Ni wazi hizi nguvu sio za kawaida, wananchi wamejitokeza wengi, wengi sana. Walianza kukusanyika tokea asubui. Mimi nilikuwa sijui kuna nini ila nilipoanza kuwauliza moja moja ili nipate kujua kuna nini, wote walinijibu wamekuja katika safari ya matumaini na kweli baada ya kuona uwingi ule wa watu sina neno zaidi ya kusema HII NDIO SAFARI YA MATUMAINI"... Emmanuel..
Mafuriko haya ya watu ni kiashiria tosha ya jinsi gani wananchi wameamua kuunga mkono safari ya matumaini. Safari ambayo Nchi itapata uongozi wenye uthubutu, usioogopa kufanya maamuzi magumu, uongozi thabiti, makini na usioyumba. Uongozi wenye ubunifu na upeo mkubwa, uongozi unaoamini katika mfumo shirikishi katika ujenzi wa Taifa na uongozi unaozingatia muda katika kutekeleza majukumu yake. Ndugu yangu wakati ndio huu, njoo ujiunge na safari ya matumaini....
"HII NDIO SAFARI YA MATUMAINI, MCHAKAMCHAKA WA MAENDELEO"....
Page 1 of 1
Permissions in this forum:
You cannot reply to topics in this forum
|
|
Sun Oct 25, 2015 7:59 pm by Admin
» Upinzani Tanzania wazindua kampeni
Sat Aug 29, 2015 8:11 pm by Admin
» Joke Of the Day
Sun Jun 07, 2015 12:53 pm by Admin
» Tatizo sugu LA Ajira
Sat Jun 06, 2015 7:29 pm by Admin
» Joke Of the Day
Sat Jun 06, 2015 7:28 pm by Admin
» Joke Of the Day
Sat Jun 06, 2015 7:26 pm by Admin
» * MAFURIKO MAKUBWA YATOKEA MWANZA....
Sat Jun 06, 2015 12:35 pm by Admin
» Lakini ungeweza Kama ungetaka
Wed Jun 03, 2015 1:03 pm by Admin
» Fun fact teehe
Wed Jun 03, 2015 8:21 am by Admin